Tuesday, May 23, 2017

Dawa za Asili za Mimea (Kuzuia Wadudu Waharibifu wa Mazao)

Unaweza kutumia mimea fulani kupunguza idadi ya wadudu waharibifu shambani mwako. Panda mimea ambayo huepukwa na wadudu waharibifu karibu na mimea inayohitaji kulindwa. Kwa mfano, minyoo fulani ambayo hula na kudhoofisha mizizi ya mimea mingi haiwezi kukaribia mimea ya matageta. Na vipepeo fulani ambao huharibu kabichi hawakaribii kabichi zilizopandwa karibu na mimea ya rosemary, sage, au thyme.Hata hivyo, tahadhari hii yafaa: Mimea fulani huwavutia wadudu waharibifu.
JINATIBAUTUMIAJI
MnyaaKuua MchwaMatone 10 ya mnyaa + maji lita moja. Koroga. Nyunyuzia/ Pulizia kwenye mchwa
UtupaWadudu wanaoshambulia mbogaTwanga kiganja kimoja cha majani. Loweka kwenye lita 1 ya maji kwa masaa 24. Chuja. Ongeza 1/8 ya kipande cha mche wa sabuni. Pulizia kwenye mboga
Muarobaini – MajaniWadudu wa mbogaPonda ganja mkona 1 wa majani. Changanya kwenye lita 1 ya maji. Loweka kwa siku mbili , halafu ongeza sabuni 1/8 ya kipande mche. Nyunyuzia kwenye mboga.
Muarobaini - MbeguWadudu wanaoshambulia mbogaTwanga mbegu kilo 5 (kisado kimajo). Loweka kwenye maji lita 15 kwa masaa 24. Chuja na pulizia/ nyunyuzia kwenye mboga
PapaiKuua mchwa Ponda majani laini ya mpapai.Ongeza lita 1 ya maji. Chuja na pulizia/ nyunyuzia kwenye mchwa
Bangi MwituKuhifadhi vyakula vya nafaka (food grains)Sambaza halafu weka gunia juu yake. Endelea hivyo hivyo.
Mkojo wa n’gombeKuua mchwa/ wadudu wa mbogaUache mkojo kwa siku 10 –14. Kwa kila lita 1 ya mkojo ongeza lita 2 za maji na 1/8 sabuni ya mche. Nyunyuzia kwenye mchwa au mboga
Mnanaa (mbarika mwitu)Kuua wadudu wanaoshambulia mbogaGram 100 mbegu + lita 1 maji + 1/8 sabuni mche. Pulizia/ nyunyizia kwenye mboga
Kitunguu saumuKuua wadudu wanaoshambulia mbogaGram 100 (3-4) twanga. Ongezea lita 1 ya maji. Acha kwa saa 24. Chuja na ongeza 1/8 ya kipande cha mche wa sabuni. Pulizia/ Nyunyuzia kwenye wadudu
Pilipili KaliKuua wadudu kwenye mbogaChanganya vijiko 3 vya chakula na lita 1 ya maji. Acha kwa saa 12. Ongezea 1/8 ya kipande cha sabuni mche. Nyunyizia kwenye mimea
Mashona nguoKuua waduduChemsha mbegu kikombe 1 na lita 1 ya maji kwa dakika 10 au loweka siku moja na ongezea 1/8 ya kipande cha sabuni mche. Nyunyuzia kwenye mboga
Muarobaini Kideri(New Castle disease)Twanga majani 1kg, ongeza maji lita 1. Wanyweshe kuku asubui. Fanya hivi kila mwezi
MajivuKuua wadudu mafuta (aphids)Nyunyizia majivu kwenye wadudu wanaoshambulia mboga
MajivuKuhifadhi mazaoChanganya majivu + pilipili kichaa + Cyprus. Sambaza kwenye gunia halafu weka gunia juu yake. Endelea hivyo hivyo.
MarejeaMboleaPanda shambani na baadaye limia chini ardhini

No comments:

Post a Comment